http://kariakoodsm.blogspot.com
KARIAKOO BLOG:Kwa Habari Kali Za Mjini | SIASA | BURUDANI | UCHUMI | FASHION | BLOGGER TRICKS | UDAKU | MICHEZO | WASILIANA NA MIMI|0713305567 |urassaombeni@yahoo.com|KWA| MATANGAZO| BABARI| USISITE PIA KUCOMMENT KWENYE HABARI ZETU | <div style='background-color: #de24de;'><a href='http://www.ikiloop.com/' title='link'></a></div>
Showing posts with label BREAKING NEWS. Show all posts
Showing posts with label BREAKING NEWS. Show all posts

Tuesday, 28 May 2013

HABARI ZAIDI JUU YA KIFO CHA MANGWEAR:


Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.

Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia leo. 

Hussein Original ambaye yupo Pretoria amesema Ngwear na   M to the P  ambaye walikuwa room moja  wamekutwa wamezima   baada  ya  kuzidhisha  madawa  ya  kulevya...

Hata hivyo mwenyeji wa rapper Albert Mangwea aliyefariki leo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, amesema hit maker huyo wa Mikasi amefariki akiwa usingizini.

Akiongea na mwandishi wetu  muda mfupi uliopita, mwenyeji huyo aitwaye Jonathan amesema usiku wa kuamkia leo Mangwair alirudi nyumbani alikofikia akiwa mzima wa afya lakini mpaka kunakucha hakuonesha dalili za kuamka.


Ameongeza kuwa asubuhi kulipokucha aliondoka na  kuendela na mishemishe yake na alipokuwa huko wenzake walimpigia simu kumtaarifu kuwa wamempeleka hospitali ya St. Helen ya jijini humo kwakuwa alikuwa bado hajaamka na ndipo walipogundua kuwa ameshafariki.

Jonathan  amesema hakuweza kujua sababu za kifo cha Ngwair kwakuwa maelezo ya daktari yalikuwa kitaalam kiasi cha kushindwa kuelewa. Ngwair alikuwa amepanga kurudi leo nchini.


Taarifa za kifo cha Ngwair zimepokelewa kwa mshtuko na watu na makampuni mbalimbali nchini yametuma salamu za rambi rambi kupitia kwenye mitandao ya kijamii.


Kilimanjaro Lager ‏
Umeondoka wakati bado tasnia ya muziki inakuhitaji. Pumzika kwa Amani Albert Mangwea “Cowwizy”.


Ndovu Special Malt
R.I.P Albert Mangweir! You will be missed by many Tanzanians. 


Adam Nditi 
Yani siamini Mangwear amefariki dunia nini ilichomkuta #RIP #Mangwair #akaCowbama


Diva ‏
Jamani Ngwair , am in tears now ….. Jamani!. I can’t believe this. I can’t tweet The RIP….. Whyyyyy?

Sunday, 5 May 2013

MWENDELEZO WA KINACHOENDELEA ENEO LILILOTOKEA MLIPUKO ARUSHA


MUDA MFUPI BAADA YA MLIPUKO KUTOKEA KILA MTU AKIKIMBIA KUOKOA MAISHA YAKE
DSCN2226
DSCN2227
Hali ya eneo mlipuko ulipotokea
DSCN2220
Waumini na wananchi wengine wakiwa na shauku ya kujua kilichotokea
DSCN2228
Ulinzi umeimarishwa
DSCN2252
Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi.
DSCN2246
Wanasualama Mkoa wa Arusha, wakijadiliana jambo katika eneo la tukio
DSCN2282
Meya wa Manispaa ya Arusha, Mh gaundence Lyimo akielekea eneo la tukio kwa miguu baada ya utaratibu wa kutumia magari kuwa mgumu kutokana na idadi kubwa ya watu na magari yaliyoziba njia.
DSCN2258
Magesa Mulongo akiteta na RCO wa Mkoa wa Arusha
DSCN2273
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, magesa Mulongo akijiandaa kuzungumza na wananchi kanisani hapo na kuahidi kuwa Serikali itahakikisha watu wote waliohusika na jaribio hilo ovu, pamoja na mtandao wao wanakamatwa. Alidai pia vikosi vya Jeshi maalumu kwa kuchunguza milipuko vitafika eneo hilo ili kufanya uchunguzi. Taarifa za eneo la tukio zinaeleza kuwa tayari kuna mshukiwa mmoja ameshatiwa mbaroni na yuko mikononi mwa Jeshi la Polisi kwa mahojiano na uchunguzi zaidi. 
DSCN2236
Eneo lenye utepe ndipo kitu hicho kinachodhaniwa kuwa bomu kilipoangukia. Pichani unaweza kuona wigi za kichwani na viatu vya waumini vikiwa vimesambaa baada ya wenyewe kuviacha, miongoni mwao wakiwa ni majeruhi.
DSCN2251
DSCN2267
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo akizungumza na mmoja wa mapadri wa Kanisa hilo kupewa maelezo ya kuhusu kilichotokea kanisani hapo.
DSCN2276
DSCN2255
DSCN2281
DSCN2225
DSCN2222
DSCN2215
DSCN2218

PICHA NA MATUKIO MBALIMBALI KANISA LILILOLIPULIWA NA BOMU ARUSHA

eneo lenye utepe ndipo kinachohisiwa kuwa bomu ndipo kilipotua na kulipuka katika Kanisa la Mt Joseph Olasiti Arusha ambapo Balozi wa Papa alikuwa akihudhuria ibada ya Kuzindua Parokia kanisani hapoMungu uwe upande wetu
Umati wa wakazi wa Arusha wakielekea eneo la tukio kujua hali za ndugu zako

ARUSHA UPDATES: RPC- ARUSHA ATHIBITISHA KUWA KILICHOLIPUA KANISA NI BOMU



Mkuu wa Mkoa Mulongo naye  amefika  eneo  la  tukio  na  kuwafariji  wahanga  wa  tukio  la  bomu....

RPC  wa  mkoa  wa  Arusha  naye  aliambatana  na  mkuu  wa  mkoa  na  muda  huu  alikuwa  anatoa  nasaha  zake  kwa  wananchi....

RPC  ameeleza  kuwa  tukio  hili  ni  la kigaidi. Katika  maelezo  yake, RPC amesema kuwa  aliyehusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu. ...

Amesema Polisi wanawasaka waliohusika  na  unyama  huu  na  ameomba yeyote  mwenye taarifa yoyote aisaide polisi. ..


Waliojeruhiwa ni 50 .Hao wana majeraha ya kawaida  na 3 wako  mahututi

Mpaka sasa  mtu mmoja anashikiliwa  na  polisi kwa mahojiano  zaid

ARUSHA UPDATES: MBUNGE LEMA ATEMBELEA ENEO LA KANISA LILILOLIPULIWA


Godbless  Lema ambaye  ni  mbunge  wa  arusha  ametembelea  eneo  la  kanisa  lililolipuliwa  na  kuwafariji  wahanga  wa  tukio  hilo.....

 Akiongea  kwa  jazba  na  hasira  na  wanachi  waliopo  eneo  la  tukio,Lema  ameitumu  serikali  kwa  mara  nyingine  na  kudai  kuwa  uzembe  wa  viongozi  ndo  chanzo  cha  matukio  kama  haya....

Hotuba  fupi  na  nasaha  zake  zilikuwa  zikisikika  moja  kwa  moja  kupitia  Radio  maria   kabla ya  kituo  hicho  kuamua  kukatisha  nasaha  zake.....

Haijafahamika  mara  moja  sababu  za  kukatishwa  kwa  hotuba  yake ...

Bado tunasubiri  taarifa  rasmi  ya  vyombo  vya  ulinzi  na  usalama  kuhusiana  na  tukio  hili

BREAKING NEWS: KANISA KATOLIKI LALIPULIWA NA BOMU JIJINI ARUSHA WAKATI MISA IKIENDELEA



Kanisa katoliki parokia ya Olasiti ambalo leo hii lilikuwa linapandishwa hadhi na kuwa Parokia limelipuliwa na kitu kinachosemekana kuwa ni bomu, watu wengi wamejeruhiwa na mtu mmoja inasemekana amefariki dunia.... ....



Tukio hilo limetokea wakati Misa ikiwa ndio inaanza .Ilikuwa ni saa 5 kamili...Kabla Askofu hajaanzisha sala , mlipuko mkubwa ulitokea ndani ya kanisa hilo......


Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa ni balozi wa Vatican nchini Tanzania. ...

Habari zaidi zinakuja

Saturday, 4 May 2013

MFANYABIASHARA AJIRUSHA TOKA GHOROFA YA TISA KARIAKOO



TAARIFA za awali zina arifu kuwa Mfanya Biashara, Costa Shirima anaedaiwa kujirusha kutoka gorofa ya tisa ya Hoteli ya Concord iliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam inaelezwa kuwa alifariki  dunia  muda mfupi  baada  ya  kujirusha na  alikuwa asafiri na ndege ya saa 10 jioni kuelekea China kufuata bidhaa za maduka yake.

Shirima (47), ambaye amefikwa na umauti muda mfupi baada ya kudondoka chini ni mfanyabiashara aliyekuwa akimiliki maduka kadhaa ya urembo wa akina mama yaliyopo jirani na Hoteli hiyo ya Concord.

Aidha taarifa hizo za awali kutoka kwa mmoja wa wanafamilia ambaye alidai kuwa si msemaji wa familia ya Shirima ya Mwika Moshi mkoani Kilimanjaro, nikuwa Marehemu mara kwamara alikuwa akipendelea kula katika hoteli hiyo na siku ya tukio inadaiwa kuwa aliwaeleza watu kuwa anapanda juu ya Hoteli hiyo kupunga upepo baada ya kuhisi hewa nzito mahali alipokuwa.


Inadaiwa kuwa baada ya kupanda huko juu ghafla alianguka chini na kudondokea gari dogo aina ya Toyota Corola linalofanya biashara ya Taxi na kupoteza maisha yake na gari hilo kuharibika vibaya kutokana na kishindo hicho.

Marehemu Shirima mbali na kuwa Mfanya Biashara wa muda mrefu Kariakoo pia alikuwa akiendelea na Ujenzi wa Jengo la Gorofa maeneo ya Kariakoo.

Marehemu ameacha Mjane na watoto 5.

Wednesday, 3 April 2013

BREAKING NEWS: HALI NI MBAYA HUKO TUNDUMA....MABOMU KILA MAHALI NA WATU WAMEAMRIWA WASITOKE NJE


Masaa takribani matano mabomu ya machozi na risasi za moto zinasikika mataili yamechomwa barabarani maduka yote yamefungwa...
 Ni mshikemshike kati ya vyombo vya dola na raia hadi sasa msikiti mmoja umechomwa moto maeneo ya mwaka na kisimani  
Hali ni mbaya zaidi kwan mabomu ya mochozi yanapigwa hadi vyumbani. 
Imetollewa amri watu wote walale majumbani kwao
Chanzo  cha  tatizo  ni  waislam  na  wakristo.Wametofautiana  juu  ya  swala  la  kuchinja.

STAY TUNED: MORE NEWS TO COME