http://kariakoodsm.blogspot.com
KARIAKOO BLOG:Kwa Habari Kali Za Mjini | SIASA | BURUDANI | UCHUMI | FASHION | BLOGGER TRICKS | UDAKU | MICHEZO | WASILIANA NA MIMI|0713305567 |urassaombeni@yahoo.com|KWA| MATANGAZO| BABARI| USISITE PIA KUCOMMENT KWENYE HABARI ZETU | <div style='background-color: #de24de;'><a href='http://www.ikiloop.com/' title='link'></a></div>

Monday, 21 October 2013

SIMBA WAPONEA CHUPUCHUPU KUTOKA KWA YANGA

Dar es Salaam. Bahati yao! Ndicho unachoweza kusema baada ya Simba kufanikiwa kulazimisha sare ya 3-3 dhidi ya Yanga jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mabingwa watetezi Yanga, walianza kwa kasi mchezo na kupata mabao matatu katika kipindi cha kwanza kupitia Mrisho Ngassa na mawili ya Hamis Kiiza, lakini Simba waliamka kipindi cha pili na kusawazisha mabao hayo kupitia Betram Mwombeki, Joseph Owino na Gilbert Kaze.

Katika uchunguzi uliofanywa na Gazeti hili kabla ya mchezo huo ulibaini Simba wamekuwa wakifunga mabao mengi kipindi cha kwanza na Yanga wenyewe wameruhusu mabao mengi kipindi cha pili.


Yanga waliuanza mchezo kwa kasi na dakika ya nne, ambapo katika dakika ya 14 winga Ngassa aliwainua mashabiki wa Yanga baada ya kufunga bao akiunganisha krosi ya Kiiza iliyompita beki wa Simba, Kaze.


Katika dakika ya 35, mpira wa kurusha wa Mbuyu Twite uligongwa na Kavumbagu na kumkuta Kiiza aliyeusukumia wavuni mpira huo kirahisi.Pia katika dakika ya 45, Kavumbagu aliwatoka mabeki wa Yanga na kupitisha krosi fupi kwa Kiiza aliyefunga bao la tatu kirahisi.


Kocha wa Simba, Abdallah Kibaden atajutia uamuzi wake wa 4-4-2 kwa kuwaanzisha Chanongo, Singano, walioshindwa kurudi katikati kuwasaidia Humoud na Mkude kulinda kutokana na kuzoea kucheza kama winga.


Yanga walikuwa imara zaidi katikati ya uwanja wakiwa na viungo watatu Athuman Idd, Frank Domayo na Haruna Niyonzima pamoja na Kavumbagu aliyesaidia hivyo kuwafanya kuwa wanne na kuwafunika kabisa Mkude na Humoud.

Hata hivyo kipindi cha pili katika dakika ya 47 Kibaden aliwapumzisha Chanongo na Humoud na kuwaingiza Said Hamis Ndemla na William Lucian walioimarisha safu ya kiungo na kuirudisha Simba mchezoni.

Mshambuliaji Mwombeki aliipatia Simba bao la kwanza katika dakika ya 53, baada ya mabeki wa Yanga, Nadir na Yondani kufanya uzembe wa kumkaba Amis Tambwe na kutoa nafasi kwa mfungaji .


Dakika ya 57, Owino aliipatia Simba bao la pili akiunganisha kwa kichwa kona ya Singano kufanya matokeo kuwa 3-2.

Baada ya hali hiyo, kocha wa Yanga, Brandts alimtoa Kiiza na kumwingiza Simon Msuva, ambapo katika dakika ya 64 Ngassa alpiga shuti la karibu lililopanguliwa na kipa Abel Dhaira.

Yanga imeendeleza udhaifu wa kuruhusu mabao katika kipindi cha pili kwani kati ya mabao saba waliyofungwa msimu huu kabla ya jana, waliruhusu kuanzia katika dakika ya 49 mpaka 90, ndicho kilichotokea, baada ya Kaze kumalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Cholo katika dakika ya 83 na kuiandikia Simba bao la kusawazisha. baada ya mechi kumalizika, kocha wa Simba, Abdalah Kibaden aliwasifu wachezaji wake kwa kucheza kwa kujituma na kufanikiwa kusawazisha.

Naye Brandts alisema wachezaji wake walicheza kizembe kipindi cha pili hasa sehemu ya kiungo.

Yanga iliwasili uwanjani saa 8:33, kupitia mlango wa kawaida, wakati watani zao Simba waliingia saa 8:35 kwa kupita geti lililopo upande Kaskazini walipo mashabiki wao.

Katika mchezo wa awali wa timu za vijana, Simba B na Yanga B zilimaliza kwa kutoka sare 1-1.


Vikosi

Simba: Abel Dhaira, Nassor ‘Cholo’ Masoud, Haruna Shamte, Kaze Gilbert, Joseph Owino, Jonas Mkude, Abdulhalim Humoud/ Lucian William, Ramadhani Singano, Amisi Tambwe, Betram Mwombeki/ Zahoro Pazi na Haruna Chanongo/ Said Hamisi.

Yanga: Ally Mustapha ‘Barthez’, Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Mrisho Ngassa, Frank Domayo, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza/ Simon Msuva na Haruna Niyonzima

KAULI NZITO YA SOFIA SIMBA: SUGU ANA MAPEPO!!!



Mbeya. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT), Sofia Simba na Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa waMbeya, Dk Mary Mwanjelwa (CCM), juzi walitumia muda mwingi jukwaani kumnangaMbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Chadema) wakimfananisha na `pepo’ aliyekwenda bungeni kwa ajili ya kufanya vurugu.
Mbeya. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT), Sofia Simba na Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa waMbeya, Dk Mary Mwanjelwa (CCM), juzi walitumia muda mwingi jukwaani kumnangaMbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Chadema) wakimfananisha na `pepo’ aliyekwenda bungeni kwa ajili ya kufanya vurugu.
Viongozi hao walisema kuwa wananchi wa jiji hilo wamepeleka ‘pepo’ bungeni ndio maana mbunge  huyo amekuwa kinara wa vurugu ndani ya Bunge, hivyo wananchi wa Mbeya Mjini wamempeleka mtu anayehitaji kuombewa.
Walitoa kauli hiyo juzi wakati wakihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la wazi la Kata ya Manga
Mjini Mbeya.
Simba, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, alisema hali hiyo ya ‘mapepo’ mara kadhaa imekuwa  ikimsababishia mbunge huyo kujiingiza kwenye vitendo vya vurugu, likiwemo tukio la hivi karibuni kupigana bungeni badala ya kuibua hoja za maendeleo. Juhudi za gazeti hili za kumtafuta Sugu zilikwama jana baada ya kuelezwa na watu wake wa karibu kuwa alikuwa safarini China.
Simba alisema tukio la mbunge huyo kupigana na askari wa bunge ndani ya ukumbi, lilitokea kwa kuwa hakukuwa na mtu wa kuombea ‘mapepo’ siku hiyo baada ya kumkumba ghafla mbunge huyo.
 “Siku ile tukio linatokea bahati mbaya sana  Mchungaji  Lwakakatare (Mbunge  wa Viti Maalumu Getrud Lwakatare) hakuwemo ukumbini maana angeweza kuyaombea na hivyo naomba wananchi wa Mbeya msituletee ‘mapepo,” alisema.
Viongozi hao walisema kuwa wananchi wa jiji hilo wamepeleka ‘pepo’ bungeni ndio maana mbunge huyo amekuwa kinara wa vurugu ndani ya Bunge, hivyo wananchi wa Mbeya Mjini wamempeleka mtu anayehitaji kuombewa.

Walitoa kauli hiyo juzi wakati wakihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la wazi la Kata ya Manga

Mjini Mbeya.

Simba, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, alisema hali hiyo ya ‘mapepo’ mara kadhaa imekuwa ikimsababishia mbunge huyo kujiingiza kwenye vitendo vya vurugu, likiwemo tukio la hivi karibuni kupigana bungeni badala ya kuibua hoja za maendeleo. Juhudi za gazeti hili za kumtafuta Sugu zilikwama jana baada ya kuelezwa na watu wake wa karibu kuwa alikuwa safarini China.

Simba alisema tukio la mbunge huyo kupigana na askari wa bunge ndani ya ukumbi, lilitokea kwa kuwa hakukuwa na mtu wa kuombea ‘mapepo’ siku hiyo baada ya kumkumba ghafla mbunge huyo.

“Siku ile tukio linatokea bahati mbaya sana Mchungaji Lwakakatare (Mbunge wa Viti Maalumu Getrud Lwakatare) hakuwemo ukumbini maana angeweza kuyaombea na hivyo naomba wananchi wa Mbeya msituletee ‘mapepo,” alisema.

Saturday, 19 October 2013

Thursday, 17 October 2013

KAULI YA ZITTO KABWE YAVIAMSHA VYAMA VYA SIASA: WENGINE WAANZA KUJISAFISHA


Dar es Salaam. Maelekezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe kutaka kusitishwa kwa ruzuku kwa vyama vya siasa nchini kutokana na kutowasilisha taarifa za ukaguzi wa matumizi yake, yamevivuruga baadhi ya vyama vilivyotajwa.


Vyama vya siasa vinaonekana kutoa matamshi yanayolenga kujinasua katika hoja hiyo, vikiwemo vilivyomshutumu Zitto, kuilaumu Serikali na hata vingine vimediriki kutaka ruzuku hiyo ifutwe kwa maelezo kwamba ni ubadhilifu wa fedha za umma.


Juzi Zitto alisema tangu 2009 Serikali ilitoa kiasi cha Sh67.7 bilioni kama ruzuku kwa vyama tisa vya siasa, lakini vyama hivyo havijawahi kuwasilisha taarifa za ukaguzi hesabu zake msajili kama sheria inavyoagiza. Kwa sababu hiyo, Zitto aliamuru Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kusimamisha utoaji wa ruzuku hadi hapo vitakapowasilisha ripoti ya ukaguzi na makatibu wake wakuu kuhojiwa.


Kwa mujibu wa Sheria namba 5 ya 1992 ambayo ilifanyiwa marekebisho ya Sheria namba 7 ya 2009, Vyama vya Siasa vinawajibika kuwasilisha hesabu zake kwa CAG na ofisi hiyo inaweza kuamua kuzifanyia ukaguzi yenyewe au kuteua mkaguzi.


Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh aliwahi kusema kuwa utaratibu ambao umekuwa ukitumiwa na vyama hivyo kwa kuteua kampuni binafsi siyo sahihi na ni kinyume cha sheria.


“Kwa mujibu wa kifungu cha 14 cha Sheria ya Vyama vya Siasa, vyama vinatakiwa viwasilishe hesabu kwa CAG, ndipo tuzikague au tuamue kampuni ya kufanya ukaguzi huo, sasa wao walichagua kampuni binafsi moja kwa moja zikawafanyia ukaguzi,” alisema Utouh wakati akitangaza kuthibitisha ubora wa hesabu za vyama vitano vilivyoshiriki kwenye Uchaguzu Mkuu wa 2010.


Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila alipendekeza kufutwa kwa ruzuku hiyo kwa vyama vya maelezo kuwa ni inawanyonya wananchi.


“Badala ya kuvipa vyama vya siasa ruzuku, tuelekeze fedha hizo kwenye miradi mingine ya maendeleo,” alisema Mtikila huku akiahidi kwamba chama hicho kitawasilisha kwa Msajili wa Vyama vya Siasa taarifa yake ya fedha iliyokaguliwa katika kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa.


CCM wang’aka


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemshambulia kiongozi huyo, huku kikisema kuwa Zitto ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema anapaswa kushughulikia matatizo yaliyopo katika chama chake kwanza kabla ya kuzungumzia matatizo katika vyama vingine vya siasa.


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema chama hicho hakihusiki na agizo la PAC la kusimaishiwa ruzuku ya kila mwezi, kwani hesabu zake zimekuwa zikifanyiwa ukaguzi. Alisema CCM ipo tayari kwenda mbele ya PAC kikiwa na hesabu zilizokaguliwa na wakaguzi wa nje, Shirika la Ukaguzi la Taifa (Tanzania Audit Corporation - TAC) kuanzia 1977/1978 hadi 2010/2011.


“Januari 29, mwaka huu niliandika barua yenye kumbukumbu namba CMM/F. 20/80/89 ili kuwasilisha rasimu ya hesabu za mwaka wa fedha 2011/2012 lengo likiwa CAG atupangie siku ya TAC kutukagua,” alisema Nape na kuongeza: “Hesabu zilizokaguliwa na wakaguzi wa nje TAC ambazo ni za 2009/2010 na 2010/2011 tayari ziliwasilishwa kwa CAG.”


Nape alifafanua kwamba hesabu za 2011/2012 bado ziko kwa wakaguzi wa nje, wakishakamilisha nazo zitawasilishwa kwenye vikao vya chama na hatimaye kwa CAG.


“Hesabu hizi zikikaguliwa kwa mujibu wa utaratibu, anapelekewa CAG ambaye ndiye anazipeleka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na sio vinginevyo,” alisema.


Alidai kuwa Zitto anapaswa kuanza kutoa ‘boriti kwenye jicho lake ndipo aone kibanzi kwenye jicho la mwenzake’ kwa sababu chama chake ndicho kimekuwa na matumizi mabaya ya ruzuku. Alisema Zitto kama Naibu Katibu Mkuu wa Chadema ni vyema akawajibika ndani ya chama chake ili kuonyesha mfano kwa wengine.


“Wote tunakumbuka kelele zilizopo mtaani kuhusu matumizi mabaya ya ruzuku zinazoelekezwa na Chadema na viongozi wake kutoka kwa wanachama wao, hivyo si ajabu wakawa wanakiuka sheria hii na ndiyo chanzo cha kelele hizo za wanachama wao,”alisema.


Vyama vingine


Kwa upande wake, Chadema kilieleza kwamba hakijapata barua inayowaarifu kuhusu kutaka kufungiwa ruzuku kutokana na kutowasilisha taarifa ya ukaguzi.


Ofisa Habari Mwandamizi wa Chadema, Tumaini Makene ilisema hata barua ya kuitwa kwenye Kamati ya PAC, iliwafikia kwa kuchelewa. “Tunasubiri barua rasmi ya suala hili ndio mamlaka zinazohusika na masuala ya fedha ndani ya chama, hususan, Baraza la Wadhamini wa Chama kuweza kutafakari hatua,” alisema Makene.


Hata hivyo, alisema angependa umma utambue kwamba “Chadema ndicho kilichokuwa mstari wa mbele tangu kabla na baada ya mwaka 2009 kutaka ukaguzi na wazi katika mapato na matumizi ya vyama vya siasa.”


Alifafanua kuwa msimamo wa Chadema kwenye mkakakati huo ulikuwa ni kuibana CCM kutokana na madai ya baadhi ya vigogo wake “kukwapua fedha Benki Kuu ( Akaunti ya Madeni ya Nje – EPA) na kuzitumia kwenye uchaguzi wa mwaka 2005.”


Alijigamba kuwa hesabu za chama chake zimekuwa zikikaguliwa kila mwaka na kwamba wanasubiri maelezo ya barua kuhusu kile kinacholalamikiwa.


Kwa upande wa Chama cha Wananchi (CUF) kimesema hesabu zake ziko safi, ila imeshindikana kukaguliwa kwa vile Serikali haijatoa fedha za kugharimia ukaguzi huo.


Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Tanzania Bara, Julius Mtatiro alisema hesabu zao zimekwishakaguliwa na wakaguzi wa ndani.“Tunachosubiri ni Serikali kutuletea mkaguzi ambaye baada ya kufanya hivyo hesabu zetu zitakuwa zimekamilika na wananchi wataweza kuziona,” alisema.


Alisema chama hicho hakina fedha kwa ajili ya kugharimia mkaguzi wa nje na kwamba jukumu hilo ni la Serikali.


Naye Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Samwel Ruhuza alisema kuwa chama hicho kipo tayari kuwasilisha hesabu zake, kwani zipo tayari na kwamba walishindwa kuziwasilisha baada ya kuelezwa kuwa CAG ndiye anayepaswa kufanya ukaguzi.


Imeandaliwa na Aidan Mhando, Leon Bahati, Fidelis Butahe na Raymond Kaminyoge

Wednesday, 16 October 2013

TUBURUDIKE KIDOGO JAMANI

PICHA ZA RED KAPET BET AWARDS 2013

2 Chainz Kwenye Tuzo za BET Hiphop Music Awards jana, 
B.o.b
Eve 
CLICK READ MORE KUCHEK ZAIDI MTU WANGU
Kevin Hart

Nelly

Rick Ross

Snoop Dogg

Schoolboy Q, Kendrick Lamar, & Jay Rock

Bone Thugs-N-Harmony 

Future & Mike Will

Lee On The Beats, DJ Khaled, & Ace Hood



Lil Mama

NILIVYOTESWA NA NILIYEMPENDA NA HATIMAYE AKAPIGWA MTUNGO


Zamani nilikuwa nasikia tu stori za kisekondari juu ya haya mambo lakin kweli wahenga walisema kuwa uyaone.


Nilikuwa na mchumba wangu ambaye alikuwa anasoma chuo fulani dodoma nilitokea kumpenda sana na hata kufikia hatua ya kupanga kufunga ndoa mwezi wa pili mwakani baada ya kutoa mahali mwaka huu.katika mahusiano yetu takribani miaka mitatu hatukuwai kukwaruzana kwa namna ya kutahadharisha mahusiano yetu.nilijitolea sana kumuhudumia vyema japo alikuwa na mkopo lakini pia nilikuwa ninamlipia mdogo wake wa kike ada ya diploma ktk chuo fulani par ambapo yeye anachukua diploma ya biashara.Mwaka jana mwezi wa pili nilipata safari ya kwenda nje ya nchi kufanya course ya mwaka mzima na kumuacha yeye nyumbani kwangu ambapo nilimuachia nyumba na gari yangu japo hili gari hata kabla ya sijaondoka alikuwa anatumia yy muda mwingi sababu mm nilikuwa natumia sana gari ya ofisini.mwezi wa tisa nilipewa mapumziko ya wiki mbili nikarudi na kumkuta kaleta rafiki zake watatu wanakaa pamoja mbaya zaidi hali ilinionesha kwamba walikuwa walevi wa kukubu na walikuwa wanadiliki pia kulala chumbani kwangu pindi wamelewa.niliporudi niliona nimfanyie suprise bila kumwabia kumbe nilijifanyia mwenyewe maana baada ya kuwasili tz nilikaa dar siku mbili ili kuripoti nipo tz then nikaanza safari ya dom nilipofika saa kumi na mbili jioni sikumkuta nami sikupiga simu nikawanasubiri nione matokeo yake.


Sasa ilipofika saa nne usiku bado alikuwa hajarudi nikaamua kumpigia simu yangu wakati nipo nje nilikuwa natumia roaming service kwaiyo namba haikuwa nabadilika hata nilipompigia akajua bado niko nje ya nchi.cha ajabu na alichonishtua akaniambia nipo nyumbani naangalia movie nikamwambia sawa na kaka yangu kanipigiaatapita kukusalimia anatoka mwanza akasema sawa then kama baada ya dk 20 nikaona anakuja akiwa na hao wadada huku wamelewa wote nahisi sababu ya pombe hakushtuka sana aliponiona ila asubuhi aliniomba sana nimsamahe.lakini tayari kichwa changu kilishagonga alerm baada ya kuona hata mazingira halisi jinsi walivyokuwa wanaishi pale.nikawa nimerudi kumalizia course yanguna mwezi watatu nikarudi tz hapa ndipo nilipoona kuna kitu kinaendelea sio sawa.hakuwa na uhuru tena na simu yake akawa hajiamini ndipo nikaanza ku track simu yake nikagundua kabadilika sana na ana mahusiano zaidi ya mmoja nje.kilichoniuma zaidi nilipokuwa zanzibar takriban mwezi mzima kkikazi tangu mwei wa nane kumbe alikuwa kaenda club na akalewa wakambeba na wakampiga mtungo nilipopata iyo habari ikabidi niwatafute wahusika kidiplomasia na wakanipa paka mkanda waliorekodi.ijumaa nikamwambia nataka tuende kwao nikwasalimie wazazi akafurahi sana nilipofika jioni nikawaomba wote na kuanza kuwasilimulia yote na kuwaonesha mkanda kwakweli mamake alilia sana hakuamini hata huyo mwanamke hakuamini kama nilikuwa na taarifa hizo zote nikawa nacheka nae hivi nimerudi jana wakuu na kuona nishare nanyi kwa mawali matatu